Tuesday, May 8, 2012

Mfumo Mpya wa Sheria za Ardhi



Waashiki wa sheria watakubaliana nami kuwa mfumo wa sheria umebadilika kufuatana na kupitishwa sheria mpya za ardhi.
Rais aliziidhinisha miswada hii na kuzifanya kuwa sheria tarehe 27 Aprili 2012:

v  Land Act (No. 6 of 2012);

v  The Land Registration Act (No. 3 of 2012); na

v  The National Land Commission Act (No. 5 of 2012).

Sheria za ardhi ambazo zilikuwa zikitumika hapo awali zilikuwa:

v    The Registered Lands Act (RLA);

v    The Registration of Documents Act (RDA);

v    The Governments Lands Act (GLA);

v    The Indian Transfer of Property Act (ITPA);

v    The Land Titles Act (LTA);

v    The Registration of Titles Act


Baadhi za lawama ambazo zimekuwa zikilimbikiziwa sheria za ardhi za hapo awali ni kuwa zilikuwa zimezagaa hivi kwamba aliyetaka kuzichunguza angetatizika. Wanasheria na mawakili ambao walifaa kutumia fomu na kuandika mikataba ya ardhi hawakufurahia hali hiyo. Hivyo basi, sheria hizi mpya ni jambo zuri.

Katika makala yatakayofuata, nitaangazia baadhi za kasoro za sheria hizi mpya na kutoa ulinganisho na mifumo ya hapo awali.

Thursday, May 3, 2012

MARAFIKI WA VITABU

Itanibidi nihifadhi blogu ambayo nimegundua leo hapa ili nisiisahau.

Hii blogu ina taarifa nzuri kwa wale wanaopenda vitabu.

Link yake ni Marafiki wa Vitabu.

Asante.

Friday, April 20, 2012

Elewa Katiba Yako: Makala ya Kwanza



Baada ya kusomea taaluma ya Sheria kwa muda mrefu, inanipasa kuelimisha jamii kuhusu masuala ya sheria ambayo yanawatatanisha ama hawajapata fursa ya kuzisoma. Mwanzo, mtaniruhusu kudurusu vipengele muhimu yanayohusu bunge. Kuelewa bunge ndiko kuelewa jinsi ambavyo inaendesha masuala yake na matarajio yako mwananchi kwa wajibu unaomkabidhi kwa kumchagua.

Imenibidi kuwasilisha ujumbe huu kwa Kiswahili kwa sababu lugha ya mkoloni si wengi wanaizungumza na kuielewa. Pia, elimu kwa umma inapaswa kuwa kwa lugha inayoeleweka kwa urahisi.

Muhtasari:

Katiba ya Jamhuri ya Kenya inazungumzia suala la Bunge katika Sura ya nane kuanzia kipengee cha 93 hadi 128. Imegawanywa katika sehemu sita.

Sehemu mbali mbali

Sehemu ya Kwanza— Kuundwa na jukumu la Bunge
Sehemu ya Pili— Wanachama wa Bunge
Sehemu ya Tatu—  Maafisa wa Bunge
Sehemu ya Nne— Taratibu za kupitisha sheria
Sehemu ya Tano—Taratibu na sheria za Bunge
Sehemu ya Sita- Ziada

Haya basi twende moja kwa moja hadi Sura ya Nane.

~

SURA YA NANE
BUNGE

Kuundwa kwa Bunge
93.     (1) Kuna Bunge buniwa la Kenya litakalojumuisha Bunge na Seneti.
          (2) Bunge na Seneti zitatekeleza majukumu yao kwa mujibu wa katiba hii.


Jukumu la Bunge
94.    (1) Jukumu la kutunga sheria la Jamhuri hii katika kiwango cha kitaifa ni la             Bunge.
(2) Bunge hutokeza tofauti za kitamaduni katika taifa, linawakilisha maoni ya
watu na hutekeleza mamlaka yake.
……

Jukumu la Bunge
95.     (1) Bunge linawakilisha watu wa maeneo bunge na matakwa muhimu katika Bunge.
          (2) Bunge lina uwezo wa kupitisha sheria kulingana na sehemu ya 4 katika sura hii.
          (4) Bunge lina jukumu la—
(a)   kuidhinisha kugawana kwa mapato miongoni mwa viwango    mbalimbali vya  serikali na miongoni mwa serikali zenyewe katika kila kiwango na kukadiria hazina ya gharama ya serikali ya kitaifa na taasisi nyingine za Serikali ya kitaifa kwa mujibu wa Sura ya Kumi na Mbili;
(b) kutenga fedha za matumizi za serikali ya Kitaifa na sasi zingine za Taifa;
 (c) kufuatilia kuona iwapo kumekuwa uwazi katika matumizi ya rasilmali za kitaifa.
          (5) Bunge lina jukumu la—
(a) kuchunguza utendakazi wa ofisi ya Rais, Naibu wa Rais na maofisa wa Serikali na ikiwezekana kuanzisha hatua za kuwatoa ofisini; na
(b) kuchunguza kwa makini na kusimamia hatua zinazochukuliwa na taasisi za Serikali.
(6) Bunge lina mamlaka ya kuidhinisha matangazo ya vita na kuendelezwa kwa tangazo la muda wa hali ya hatari.

Jukumu la Seneti
96.  (1) Seneti linawakilisha kaunti, na litashughulikia masuala ya kaunti za serikali zao.
      (2) Seneti litashiriki katika kukusanya na kutunga sheria ya kitaifa na kulinda maslahi ya        serikali hiyo iliyogatuliwa kwa mujibu wa vipengee vya 109 hadi 113.
    (3) Seneti litashughulika na kutenga fedha za matumizi za serikali ya Kitaifa katika serikali iliyogatuliwa kwa mujibu wa kipengee cha 217, na kuchunguza kwa makini matumizi za pesa za serikali.
   (4) Seneti litajishirikisha  katika uchunguzi wa makini wa Maafisa wa Serikali, kuchunguza utendakazi wa ofisi ya Rais au Naibu wa Rais na ikiwezekana kuanzisha hatua za kuwatoa ofisini kwa mujibu wa kipengee cha 145.

~
Itabidi nikome hapo kwa leo. Katika makala mengine, nitatathmini vipengele vingine vilivyomo ndani ya Katiba.

Nikisoma Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Jumuiya ya Tanzania, nimefurahishwa na jinsi ambavyo wametumia lugha ya Kiswahili haswa katika haya:

     i.        Kwa madhumuni ya ufafanuzi wa masharti ya ibara hii neno "…." Maana yake ni….
   ii.        Bila ya kujali masharti ya ibara ndogo ya (1),….
 iii.        Ibara kwa kiingereza ni Section.
  iv.        Misingi ya Katiba kwa kiingereza ni Preamble.

Thursday, April 19, 2012

Nimerudi


Wasomaji wangu,

Kwanza lazima nitoe msamaha wangu wa dhati kwa kutulia kwa kipindi cha muda mrefu. Nimerudi kwa kishindo na nimeandaa makala muhimu ambayo yanaelezea baadhi ya mambo ambayo ninayaona kuwa muhimu.

Tegea makala yangu baada ya muda mfupi.

Wasaalam,
Lorot