Tuesday, May 8, 2012

Mfumo Mpya wa Sheria za Ardhi



Waashiki wa sheria watakubaliana nami kuwa mfumo wa sheria umebadilika kufuatana na kupitishwa sheria mpya za ardhi.
Rais aliziidhinisha miswada hii na kuzifanya kuwa sheria tarehe 27 Aprili 2012:

v  Land Act (No. 6 of 2012);

v  The Land Registration Act (No. 3 of 2012); na

v  The National Land Commission Act (No. 5 of 2012).

Sheria za ardhi ambazo zilikuwa zikitumika hapo awali zilikuwa:

v    The Registered Lands Act (RLA);

v    The Registration of Documents Act (RDA);

v    The Governments Lands Act (GLA);

v    The Indian Transfer of Property Act (ITPA);

v    The Land Titles Act (LTA);

v    The Registration of Titles Act


Baadhi za lawama ambazo zimekuwa zikilimbikiziwa sheria za ardhi za hapo awali ni kuwa zilikuwa zimezagaa hivi kwamba aliyetaka kuzichunguza angetatizika. Wanasheria na mawakili ambao walifaa kutumia fomu na kuandika mikataba ya ardhi hawakufurahia hali hiyo. Hivyo basi, sheria hizi mpya ni jambo zuri.

Katika makala yatakayofuata, nitaangazia baadhi za kasoro za sheria hizi mpya na kutoa ulinganisho na mifumo ya hapo awali.

No comments:

Post a Comment