Friday, April 20, 2012

Elewa Katiba Yako: Makala ya Kwanza



Baada ya kusomea taaluma ya Sheria kwa muda mrefu, inanipasa kuelimisha jamii kuhusu masuala ya sheria ambayo yanawatatanisha ama hawajapata fursa ya kuzisoma. Mwanzo, mtaniruhusu kudurusu vipengele muhimu yanayohusu bunge. Kuelewa bunge ndiko kuelewa jinsi ambavyo inaendesha masuala yake na matarajio yako mwananchi kwa wajibu unaomkabidhi kwa kumchagua.

Imenibidi kuwasilisha ujumbe huu kwa Kiswahili kwa sababu lugha ya mkoloni si wengi wanaizungumza na kuielewa. Pia, elimu kwa umma inapaswa kuwa kwa lugha inayoeleweka kwa urahisi.

Muhtasari:

Katiba ya Jamhuri ya Kenya inazungumzia suala la Bunge katika Sura ya nane kuanzia kipengee cha 93 hadi 128. Imegawanywa katika sehemu sita.

Sehemu mbali mbali

Sehemu ya Kwanza— Kuundwa na jukumu la Bunge
Sehemu ya Pili— Wanachama wa Bunge
Sehemu ya Tatu—  Maafisa wa Bunge
Sehemu ya Nne— Taratibu za kupitisha sheria
Sehemu ya Tano—Taratibu na sheria za Bunge
Sehemu ya Sita- Ziada

Haya basi twende moja kwa moja hadi Sura ya Nane.

~

SURA YA NANE
BUNGE

Kuundwa kwa Bunge
93.     (1) Kuna Bunge buniwa la Kenya litakalojumuisha Bunge na Seneti.
          (2) Bunge na Seneti zitatekeleza majukumu yao kwa mujibu wa katiba hii.


Jukumu la Bunge
94.    (1) Jukumu la kutunga sheria la Jamhuri hii katika kiwango cha kitaifa ni la             Bunge.
(2) Bunge hutokeza tofauti za kitamaduni katika taifa, linawakilisha maoni ya
watu na hutekeleza mamlaka yake.
……

Jukumu la Bunge
95.     (1) Bunge linawakilisha watu wa maeneo bunge na matakwa muhimu katika Bunge.
          (2) Bunge lina uwezo wa kupitisha sheria kulingana na sehemu ya 4 katika sura hii.
          (4) Bunge lina jukumu la—
(a)   kuidhinisha kugawana kwa mapato miongoni mwa viwango    mbalimbali vya  serikali na miongoni mwa serikali zenyewe katika kila kiwango na kukadiria hazina ya gharama ya serikali ya kitaifa na taasisi nyingine za Serikali ya kitaifa kwa mujibu wa Sura ya Kumi na Mbili;
(b) kutenga fedha za matumizi za serikali ya Kitaifa na sasi zingine za Taifa;
 (c) kufuatilia kuona iwapo kumekuwa uwazi katika matumizi ya rasilmali za kitaifa.
          (5) Bunge lina jukumu la—
(a) kuchunguza utendakazi wa ofisi ya Rais, Naibu wa Rais na maofisa wa Serikali na ikiwezekana kuanzisha hatua za kuwatoa ofisini; na
(b) kuchunguza kwa makini na kusimamia hatua zinazochukuliwa na taasisi za Serikali.
(6) Bunge lina mamlaka ya kuidhinisha matangazo ya vita na kuendelezwa kwa tangazo la muda wa hali ya hatari.

Jukumu la Seneti
96.  (1) Seneti linawakilisha kaunti, na litashughulikia masuala ya kaunti za serikali zao.
      (2) Seneti litashiriki katika kukusanya na kutunga sheria ya kitaifa na kulinda maslahi ya        serikali hiyo iliyogatuliwa kwa mujibu wa vipengee vya 109 hadi 113.
    (3) Seneti litashughulika na kutenga fedha za matumizi za serikali ya Kitaifa katika serikali iliyogatuliwa kwa mujibu wa kipengee cha 217, na kuchunguza kwa makini matumizi za pesa za serikali.
   (4) Seneti litajishirikisha  katika uchunguzi wa makini wa Maafisa wa Serikali, kuchunguza utendakazi wa ofisi ya Rais au Naibu wa Rais na ikiwezekana kuanzisha hatua za kuwatoa ofisini kwa mujibu wa kipengee cha 145.

~
Itabidi nikome hapo kwa leo. Katika makala mengine, nitatathmini vipengele vingine vilivyomo ndani ya Katiba.

Nikisoma Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Jumuiya ya Tanzania, nimefurahishwa na jinsi ambavyo wametumia lugha ya Kiswahili haswa katika haya:

     i.        Kwa madhumuni ya ufafanuzi wa masharti ya ibara hii neno "…." Maana yake ni….
   ii.        Bila ya kujali masharti ya ibara ndogo ya (1),….
 iii.        Ibara kwa kiingereza ni Section.
  iv.        Misingi ya Katiba kwa kiingereza ni Preamble.

1 comment:

  1. Sorry that I can't speak Swahili well. Do you happen to know where I can get a full digital copy of the current (2010) Kenya Constitution in Swahili? I can only find English copies, and a copy of an older proposed version, but not the one that went into law. Thanks.

    ReplyDelete